C8. DENTAL HEALTH TIPS FROM A DENTIST-OVERCOMING DENTAL CARIES || AFYA YA KINYWA-ZIJUE ATHARI UNAZOWEZA KUZIPATA KWA KUCHELEWA KULITIBU JINO LILILOTOBOKA/KUOZA.
Na Mwandishi Arnold Lusingo (Mwandishi ni mwanafunzi wa udaktari wa afya ya kinywa katika Chuo cha Primary health care Institute, Iringa Contacts: Twitter@kakadentine, FB: Arnold Lusingo) Rafiki, Nakukaribisha katika darasa huru na hatua nyingine ambapo tutaenda kuanagalia jinsi tunavyoweza kuimarisha afya yetu ya kinywa. Kimsingi, katika kila siku ya maisha yetu lazima tutumie kinywa ndio maana wahenga wakasema tunnza kinywa nacho kikutunze. katika utunzaji wa afya ya kinywa hakuna namna tunaweza sahau kutunza meno, hivyo basi leo tuta angalia tatizo sugu la meno kutoboka au kuoza. Tunza kinywa nacho kikutunze Ø Jino lililooza au kutoboka ni jino gani? Ni jino ambalo limepoteza madini yake na kuwa na tundu katika sehemu moja au zaidi ya jino ambayo hii husababishwa na kazi inayofanywa na bakteria (fukuo) kutengeza asidi(tindikali). Kwa jina la kitabibu kutoboka au kuoza kwa jino huitwa Dental Caries. Ø Ni nini hasa visababishi vya jino kutoboka/kuoza? Ili jino ...